Na Michael Komba
NDONDI ni miongoni mwa michezo ambayo imewahi kuitangaza vilivyo Tanzania katika anga ya kimataifa, kama ilivyokuwa kwa riadha.
Mabondia ambao waliwahi kuipeperusha vyema Bendera ya Tanzania katika mashindano mbalimbali ya kimataifa, ni Michael Yombayomba, Habibu Kinyogori, Titus Simba, Emmanuel Mlundwa, Rashid Matumla na wengineo.
Soka ambayo ndio mchezo unaopendwa na kupewa kipaumbele zaidi hapa nchini, haujawahi kuiletea Tanzania mafanikio yoyote, zaidi ya kushiriki fainali za Kombe la Mataifa Huru ya Afrika mwaka 1980 nchini Nigeria.
Zaidi ya mafanikio hayo, timu yetu ya Taifa, Taifa Stars na hata klabu zetu, zimebaki kuwa ‘kichwa cha mwendawazimu’ katika michuano mbalimbali ya kimataifa.
SOMA ZAIDI NGUMI