Waziri mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa(katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa viongozi wa shirikisho la waendesha bodaboda jijini Dar es Salaam ofisini kwake.Lowassa alikutana na viongozi hao kupanga utaratibu wa kufanya harambee ya kuchangia ya saccos ya shirikisho hilo.Mwezi Disemba mwaka jana Mh Lowassa alikuwa mgeni rasmi katika tamasha la bodaboda kwenye viwanja vya leaders jijini dsm ambapo aliahidi kukutana na uongozi huo kwa ajili ya kuandaa harambee ya kuwasaidia kumiliki pikipiki waendesha bodaboda wa dar es salaam.
↧